Nafasi Ya Matangazo

October 11, 2014

Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo (Oktoba 11 mwaka huu) imesikiliza malalamiko yaliyowasilishwa mbele yake dhidi ya Dk. Damas Ndumbaro.

Shauri hilo limesikilizwa na wajumbe wa Kamati hiyo chini ya Makamu Mwenyekiti wake Wakili Jerome Msemwa. Wajumbe wengine wa kamati hiyo waliosikiliza shauri hilo lililowasilishwa na TFF ni Kitwana Manara, Kassim Dau na Nassoro Duduma.

Hivyo, Kamati hiyo itakuwa na mkutano na waandishi wa habari kutangaza uamuzi wake juu ya shauri hilo. Mkutano huo utafanyika Jumatatu (Oktoba 13 mwaka huu) saa 8 mchana kwenye ofisi za TFF, Jengo la PPF Tower.
Posted by MROKI On Saturday, October 11, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo