KARIBUNI SANA KATIKA BLOGU YENU YA JAMII AMBAYO INA LENGO LA , KUELIMISHA, KUBURUDSHA NA KUKOSOA PALE INAPOBIDI BILA KUATHIRI UPANDE WOWOTE WA JAMII . MAONI YENU NI MUHIMU SANA KATIKA KUENDELEZA BLOGU HII. MAONI TUTOAYO YAZINGATIE AMANI NA UPENDO, LUGHA ZISIZOZINGATIA MAADILI YA KITANZANIA NA AFRIKA HAZIRUHUSIWI.
November 15, 2009
Hongera sana Mheshimiwa Rais... Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akimpa mkono wa pongezi Rais wa Zanzibar, Dk. Amani Abeid Karume baada ya kutunukiwa Sahada yake ya heshima ya Uzamifu kutoka Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Herbert Kairuki Dar es Salaam katika mahafali ya 7 ya chuo hicho.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Sunday, November 15, 2009 | Permalink | Maoni: 0
November 14, 2009
JK hapa mh! Uzalendo umepita kiasi Rais Jayaka Kikwete akikagua nyumba za wakzi wa Kijiji cha Msoga Wilayani Bagamoyo ambazo zimeharibiwa na mvua.

Ama kwa hakika ule usemi unasema "Mtu kwao na asiye na Kwao mtumwa" umedhihirika jana wakati Rais Jakaya Kikwete alipofanya ziara ya kukagua Nyumba kadhaa zilizoezuliwa mapaa na kuharibika vibaya katika kijiji cha Msoga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.

Kitendo hicho, hakika ni cha kizalendo na kinataka moyo wa ujasiri kukifanya hasa katika kipindi hiki ambacho taifa lipo katika msiba mkubwa.

Ndio msiba mkubwa, kwani hujui kile kilicho tokea Jumatano iliyopita katika kitongoji cha Manka, Kijiji cha Goha Kata ya Mwamba Myamba Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro.
Unakijua ila tu unataka kuntia ushahidi katika kesi yako.

Roho za watu 25 wanakadiriwa kupoteza maisha katika janga hilo kubwa kuwahi kutokea katika historia ya milima ya upareni na nchini.

Kwa maafa hayo ambayo yamepoteza si tu WAPIGA KURA bali waitikiaji wa wito na kauli mbiu ya taifa ya KILIMO KWANZA ambao ni uti wa mgongo wa taifa hili kutoka kijiji Goha.

Rais nakupongeza sana kwa kutembelea kijijini kwao na huku kwa Anne Kilango Malecela atafika yeye na DC wake Ibrahim Marwa pamoja na Mkuu wao wa Mkoa Monica Mbega.

Ninakubali kuwa hata kuezuliwa mapaa na kuharibika kwa nyumba za 'mbavu za mbwa' napo ni maafa lakini huku kwa wenzetu ni Janga kubwa maana roho za wapiga kura wenu zimetoka.

Watu wale ni juzi tu Mbunge wao aliendesha harambee ya kujenga kiwanda cha Tangawizi katika Kata yao ya Mamba Myamba, lakini sasa wakulima ndo hao wametoweka.

Mimi ni miongoni mwa watu wachache kutoka jijini Dar es Salaam ambao tumepata bahati ya kufika Kijiji cha Goha na kujionea athari hizo za maporomoko ambayo mimi naamini sio mafuriko bali kuna tetemeko dogo la ardhi lilitokea na si vinginevyo, mtaaona ripoti ya wataam wa miamba.

Mimi kwa mtazamo wangu ambao sizani kama wewe unaamini hivyo kuwa Rais Jakaya Kikwete ungeanza kwenda kuwapa pole wana Goha kwanza halafu ukarudi hapo Bagamoyo ingenipa heshima kuwa Rais wetu anatujali kwa dhiki, shida na furaha.

Huo ni mtazamo wangu tu lakini sio ukweli wa jambo lenyewe, na wala sikulazimisi kuamini kuwa JK angeanza kule ingekuwa vyema zaidi.

Lakini sio Rais peke yake hata viongozi wake wengine kama Waziri Mkuu ambaye maafa yanatokea siku kadhaa mbele huyoo anatimkia katika ziaara ya huko Lindi.

Mzee wetu Pinda kwani kulikuwa na tatizo gani kama ungefika Goha uone machozi ya wapiga kura wa Rais na Anne Kilango walivyo teketea? Naimani hata Mungu angeongeza baraka, kwani wewe Idara ya Maafa si ipo kwako?.

Ah! unaguna nini bwana kuwa sina point kwani uongo kuwa Wanagoha ni wapiga kura wa Rais na Mbunge wao Anne Kilango, Pinda wewe utaomba kura Same yanini wakati unazako huko Ruvuma.

Makamu wa Rais nawe si vibaya ukaliona hili maana wenzako wote wamezungunga muashoki na kuwaacha wapiga kura na watekelezaji wa Kilimo kwanza wameshika tama.

Jakaya sasa ni wakati muafaka kwenda Goha kuwapa pole wanakijiji maana familia nyingi zimekufa zote, na kuwapa moyo kuwa kesho ipo utarekebisha kosa la jana.

Na Huko Dodoma pia maafa yametokea yafaa twende tukawape pole sio Msoga tu nilipo zaliwa.

Nalia na wewe hadi kieleweke!

 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Saturday, November 14, 2009 | Permalink | Maoni: 0
Hii ndo Mamba Myamba kijiji cha Goha kitongoji cha MankaMrokiMroki akifanya mahojiano nma Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'hoboko katika eneo la tukio.
Eneo lililokubwa na maafa
Akina mama wakiwa kwenye majonzi katika moja ya majabali ya kitongoji cha Manka ambako maafa ya watu takriban 25 wanasadikiwa kufa.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Saturday, November 14, 2009 | Permalink | Maoni: 0
Naomi alivyotikisa Dar
Mke wa Rais mama Salma Kikwete akiwa na Mke wa rais wa Zambia Thandiwe Banda wakifuatilia onyesho onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe kwa lengo la kusaidia mpango wa uzazi salama kwa wanawake wajawazito lililofanyika kwenye Hoteli ya Movenpick usiku wa kuamkia leo jijini Dar es salaam.
Msanii na Mwanamitindo wa kimataifa Naomi Campbell akiwa jukwaani wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe kwa lengo la kusaidia mpango wa uzazi salama kwa wanawake wajawazito lililofanyika kwenye Hoteli ya Movenpick usiku wa kuamkia leo.Nyuma yake ni Bi. Rose Mlay Mratibu wa Utepe Mweupe Tanzania.
Mke wa Rais mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) akimweleza jambo Balozi wa kimataifa wa Utepe na msanii na mwanamitindo wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe.
Picha no 5.
Mke wa Rais mama Salma Kikwete akiongea na Msanii na Mwanamitindo wa kimataifa Naomi Campbell (wa pili kushoto) wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe kwa lengo la kusaidia mpango wa uzazi salama kwa wanawake wajawazito lililofanyika kwenye Hoteli ya Movenpick usiku wa kuamkia leo. Katikati ni mwanamitindo wa Face of Africa kutoka Zimbabwe Tollar Kelle.
Msanii na Mwanamitindo wa kimataifa Naomi Campbell akiongea na waandishi wa habari mara baada ya onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taasisi ya Utepe Mweupe kwa lengo la kusaidia mpango wa uzazi salama kwa wanawake wajawazito lililofanyika kwenye Hoteli ya Movenpick usiku wa kuamkia leo jijini Dar es salaam.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Saturday, November 14, 2009 | Permalink | Maoni: 0
November 12, 2009
Rais Kikwete apokea hati za Mabalozi wa Rwanda na Marekani Rais Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi mteule wa marekani hapa nchini mheshimiwa alfonso lenhardt ikulu tarehe 12.11.09. baadaye rais kikwete alifanya mazungumzo na balozi huyo.
Rais jakaya kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi mteule wa nchi ya rwanda mheshimiwa fatuma ndangiza nyirakobwa na baadaye rais kikwete alifanya mazungumzo na balozi huyo,ikulu,tarehe 12.11.09
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Thursday, November 12, 2009 | Permalink | Maoni: 0
Khatib akutana na Balozi wa NorwayWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Mhe Muhammed Seif Khatibu akisalimiana na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bw Jon Lomoy alipomtembelea Leo Ofisini Kwake Mtaa wa Luthuli Mjini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Mheshimiwa Muhammed Seif Khatibu akizungumza na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bw Jon Lomoy alipomtemelea Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli jijini Dar esSalaam leo.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Thursday, November 12, 2009 | Permalink | Maoni: 0
November 11, 2009
Ilumminata aenda China kuwania taji la Miss InternationalMiss Universe Tanzania 2009, Illuminata James, mshindi wa akiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julis Nyerere Dar es Salaam jana akienda nchini China kushiriki mashindano ya Mrembo wa Kimataifa yatakayofanyika mwishoni mwa mwezi huu katika mji wa Chengdu.
Illuminata akipozi kwa picha uwanjani hapo.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Wednesday, November 11, 2009 | Permalink | Maoni: 1
Mzee Ojjiki wa Sunderland na Mary Black Bird afariki duniaMchezaji wa zamani wa Timu ya Sunderland hivi sasa Simba, Joseph Laurence Ojjiki (77) a.k.a Msalaba, (pichani) amefariki dunia juzi jijini Dar es salaam na kuzikwa Novemba 11, 2009 katika makaburi ya Kinondoni jijini.

Ojjiki aliyezaliwa Juni 02, 1932 alifariki Novemba 08, 2009 baada ya kuugua ghafla.

Mbali na kuichezea timu ya Sunderland pia alikuwa akiichezea timu ya Taifa ya Tanganyika katika michuano ya Gossage siku hizi Challenge Cup katika mika ya 1950's.

Mbali na kulisakata gozi la Ng'ombe pia Ojjiki ni mmoja wa waanzilishi wa kundi la muziki la Mary Black Birds akiwa na Mzee Ally Sykes.

Marehemu Ojjiki ameacha watoto 3 wajukuu 12 na vitukuu 8.
Blogu hii ya jamii inawapa pole wanafamilia wote, ndugu jamaa na marafiki waliokubwa na Msiba huo mzito.
Kipekee tunaipa pole familia ya Jaji. Joseph Sinde Warioba, Familia ya Michael Maluwe na Familia ya Mwombela-Marekani.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Mungu lihimidiwe Amina.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Wednesday, November 11, 2009 | Permalink | Maoni: 1
Mamba yakubwa na mafuro 20 wapoteza maishaMafuriko makubwa yamekikumba kijiji cha Manka kilichopo Kata ya Mamba Miamba Wilayani Same mkoani Kilimanjaro na watu 20 wanaripotiwa kupoteza maisha na maelfu kupoteza makazi.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema watu waliotambulika hadi jana ni wanafunzi saba wa shule ya msingi Miamba Mamba.

Maiti waliotambuliwa ni Elitabu Shambi, Napenda Bakari, Nashemba bakari, Nati John, Mariamu Juma, Ndimangwa Elineema, Amani Mhina, Ruth Mhina, Kiondo Amani, Neema Bakari. Maiti wengine hadi jana jioni bado walikuwa hawajambuliwa.

Kijiji hicho kina watu zaidi ya 1500.
Mafuriko hayo yametokea kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo na mikoa mingine nchini. Taarifa zaidi tutaendelea kuwapa.
NB: Picha hiyo haihusiani na Mamba.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Wednesday, November 11, 2009 | Permalink | Maoni: 0
November 10, 2009
HUU NDIYO UKWELI, UZURI NA UTAMU WA BIBLIA!!Q: Sura gani ya Biblia ambayo ni fupi kuliko zote?
A: Zaburi 117

Q: Sura gani ya Biblia ambayo ni ndefu kuliko zote?
A: Zaburi 119


Q: Sura gani iliyo katikati ya Biblia?
A: Zaburi 118


Ukweli: Kuna Sura 594 kabla ya Zaburi 118Ukweli: Kuna Sura 594 baada ya Zaburi 118Ukijumlisha Namba hizi unapata 1188.


Q: Mstari upi wa katikati ya Biblia?
A: Zaburi 118:8


Q: Je Mstari huu unaongelea chochote cha maana kuhusu mpango mzima wa Mungu kwa maisha yetu?

Mara nyingine mtu akisema angehitaji kujua mpango kamili wa Mungu kuhusu maisha yake na wakati huo huo anataka kuwa katikati ya mipango yake, basi muweke mtu huyu kati ya maneno yake!(yaani usiongee kitu nje ya maneno yake)

Zaburi 118:8"Ni bora kuamini katika BWANA kuliko kumwamini binadamu." Je kwa mpangilio huu haishangazi kwa jinsi ilivyotokea (au Mungu alikuwakatikati yake)?

Kabla ya kutuma habari hii nilisali, Nilisali kwa ajili yenu. Je una dakika moja? sekunde 60 kwa ajili ya Mungu? Cha kufanya ni kusali sala ndogo kwa mtu aliyekutumia ujumbe huu.........

"Baba Mungu mpe baraka rafiki yangu kwa chochote ukijuacho kuwa yeye anakihitaji siku ya leo! Na Maisha yake yajae Amani yako, mafanikio na nguvu kama anavyohitaji kuwa karibu na wewe. Amina"

Kisha tuma kwa watu 10 wengine. Ndani ya saa utakuwa umeombewa na watu 10 wengine, utakuwa umesababisha watu wengi kuombea wenzao kwa Mungu.Kisha subiria na uone NGUVU ya MUNGU ikifanya kazi kwenye maisha yako...

Mambo yawapo Magumu, siku zote kumbuka.... Imani haikuzungushi kwenye matatizo, isipokuwa hukusaidia kuyavuka matatizo!!
Mungu Awabariki.
 
©FATHER KIDEVU | Tarehe: Tuesday, November 10, 2009 | Permalink | Maoni: 0
Idadi ya watu