Father Kidevu

Karibu!

KATIKA GAZETI TANDO HILI UTAWEZA KUJIPATIA HABARI MOTO MOTO KATIKA PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI KUTOKA NDANI NA NJE YA TANZANIA HASA YALE YANAYOGUSA MAISHA YA KILA SIKU YA MTANZANIA.LUGHA KUU INAYOTUMIKA HUMU NI KISWAHILI.


 
July 08, 2009
Bandari Dar es Salaam wacheza filamu ya mabomu.
Mkuu wa Ulinzi wa bandari akizungumza na waandishi.
Wafanyakazi wa bandari wakiingia baada ya tukio la udanganyifu wa kuwapo kwa mabomu kwisha.
Leo asubuhi wafanyakzi wa bandari ya dar es Salaam walikubwa na kizaa zaa baada ya kutangaziwa kuwapo kwa boti katika bandari hiyo ambayo inamabomu.
Kufuatia amri hiyo wafanyakzi wote walio ndani ya bandari hiyo waliamriwa kutoka nje ya eneo hilo maana ilikuwa inatakiwa kulipuliwa iwapo jitihada za kuyategua mabomu hayo zingeshindaka.

Vikosi vya uoakojai vya Zimamoto, Polisi, JWTZ na Waandishi wa habari ni miongoni mwa wawajibikaji waliofika katika eneo la tukio hilo la uigizaji.

'Mabomu' yaliyokutwa katika boti hiyo yakiwa katika gari la polisi DFP 2724.

Pichani ni matukio kadhaa ya maigizo ambayo yalifanyika baada ya mabomu hayo ambayo yalikuwa ni Matikitiki maji, Matango, Biringanya kuwekwa sawa.

Kufuatia hatua hiyo waandishi wa habari wameonya udanganyifu mkubwa uliofanya na bandari hiyo na kuwa siku nyingine linaweza tokea tukio la kweli na taarifa zisiaminike.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/08/2009 | Permalink | Maoni 0
July 06, 2009
Vijana Dow Elef International (T) LTD sabasaba
Baadhi ya Vijana wa kampuni ya uwakala ya Forodha ya upakiaji na upakuaji wa mizingo bandarini, viwanja vya ndege na mipakani Dow Elef International (T) LTD wakiwa katika picha ya pamoja katika ofisi yao iliyopo viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa Dar es Salaam.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/06/2009 | Permalink | Maoni 0
July 05, 2009
Fadhili na Shufaa walivyo meremeta
Bwana Fadhili Akida na Mkewe Bi. Shufaa wakiwa katika nyuso za furaha wakati wa tafrija ya kuwapongeza iliyofanyika Julai 4 2009 katika ukumbi wa Msasani Club Dar es Salaam.
Shufaa akiweka alama ya ndoa yao kwa kumvisha pete Fadhili.
Fadhili akimvisha pete mkewe Shufaa.
Mziki ulifunguliwa mapema na watu walianza kujirusha mduara hadi basi.
Pius Ntiga akitoa pongezi.
Kyao Hoza akigonga glasi kuwatakia heri maaharusi.
Doble G akigonganisha glas wakati wa tafrija hiyo.
Wakwe wakijisevia msosi.
Marafiki wa Fadhili Akida kutoka kushoto, Athuma, Zamzam na Gondwe.
Marafiki ambao pia ni wafankazi wenzake na Fadhili katika tasnia ya Habari wakiyarudi magoma wakati wa zawadi. Kutoka kushoto ni Pius Ntinga wa Uhuru FM, Godwin Gondwe wa Redio One, Mrs Mroki na Father Kidevu wa Habarileo.
Hapa ni katika picha ya pamoja.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/05/2009 | Permalink | Maoni 0
DJ wa Mlimani Redio akiwa kazini.
DJ G wa Redio Mlimani akifanya vitu vyake leo katika Banda la Maonesho ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. DJ G yupo mwaka wa pili katika Taasisi ya Habari na Mawasiliano ya Umma (IJMC).
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/05/2009 | Permalink | Maoni 1
Sabasaba Leo
Idadi ya watu katika viwanja vya maonesho ya sabasaba barabara ya Kilwa Dar es Salaam leo imezidi kuongezeka na watu ni wengi katika mabanda na barabara za mitaa yote. Watu wanapaswa kuwa waangalifu hasa wale wanaoingia na watoto na hata mali zao upande wa mifukoni.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/05/2009 | Permalink | Maoni 0
July 04, 2009
Mbilia Beli alivyo pagawisha Dar es Salaam.
Mwanamuziki kutoka Jamhiri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akimpagawisha mmoja wa mashabiki waliohudhuria onyesho lake lililofanyika Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oyster bay jijini Dare es Salaam mwishoni mwa wiki. Shoo hiyo iliandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania. Mbilia Bel, akiwaongoza wacheza shoo wake Getrude Zongo(katikati) na Sheila Juma (nyuma) kushambulia jukwaa wakati wa shoo iliyofanyika Ijumaa usiku katika Bwalo la Maofisa wa Police Oysterbay jijini Dar es Salaam. Shoo hiyo iliandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Zain Tanzania.
Mbilia Bel, akiungana na wacheza shoo wake kushambulia jukwaa wakati wa shoo iliyofanyika Ijumaa usiku katika Bwalo la Maofisa wa Police Oysterbay jijini Dar es Salaam. Shoo hiyo iliandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Zain Tanzania.
Wacheza shoo, Sheila Juma (kushoto) na Aisha Abdallah wakionyesha umahiri wa kucheza rhumba wakati mwanamuziki kutoKA Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel alipokuwa akitumbuiza mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam. Onesho hilo liliandaliwa na Zain Tanzania.
Mashabiki wa musiki wakiwa wamevamia steji wakati wa Mwanamuziki nguli kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza mwishoni mwa wiki katika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Shoo hiyo iliandaliwa na kampuni ys mawasiliano ya simu za mkononi ya Zain Tanzania.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/04/2009 | Permalink | Maoni 1
Miss Vodacom Vyuo vya Elimu ya Juu 2009 katika picha
Miss Vyuo vya Elimu ya Juu 2009, Beatrice Lukindo kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) akipunga mkono baada ya kuvikwa taji hilo usiku wa Julai 3 2009.

Mrembo Dris akipita jukwaani.

Magreth Mhozya akijinadi na kivazi cha ufukweni.
Beatrice Lukindo alipojinadi na vazi la ufukweni.
Beatrice Kinyondo akipozi na vazi la ufukweni.
Jenipher Paul katika vzi la ufukweni.
Aisha Rico nae akiwa katika vazi la Ufukweni.
Doris Donatus na vazi la ufukweni.
Mwantumu Msuya akimeremeta na vazi la ufukweni.
Aisha Rico tena na vazi la jioni. Majaji wa shindano hilo wakifuatilia kwa karibu.
Tano bora iliyoingia katika hatua ya maswali katika picha ya pamoja.
Wadau kutoka Vodacom ambao ndio wadhamini wakuu wa shindano hili wakijadili jambo. Twanga Pepeta wakicheza sebene jukwaani.
Twanga tena wakiyarudi magoma. Kundi laIYF likitoa burudani
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/04/2009 | Permalink | Maoni 0
July 03, 2009
Mke wa Rais Kikwete
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiingia katika ukumbi wa mikutano wa Sirte tayari kuhudhuria kikao maalumu cha kamati ya Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya Ukimwi OAFLA, mjini Sirte Libya.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/03/2009 | Permalink | Maoni 0
Fadhili apata jiko-Shufaa apata gesi
Kambi ya Ukapera ya magazeti ya Habarileo na Dailynews imepata pigo baada ya Chipukizi wake Fadhili Akida kupata mwenza wake usiku wa kuamkia leo baada ya kufunga ndoa na Shufaa Kombo Suweid katika msikiti wa Mwinyimkuu, Magomeni, Dar es Salaam.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/03/2009 | Permalink | Maoni 0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Crown Entertainment Erasto Jones akimkabidhi zawadi ya mkufu na kidani cha madini ya Tanzanite, iliyotolewa na kampuni ya TanzaniteOne ya mjini Arusha kwa mshindi wa Shindano la Miss kanda ya Kaskazini Suzan Emmanuel.
Washindi hawa wanasuburi walimbwende wengine kutoka kanda mbalimbali katika mtanange wa kumpata Miss Tanzania 2009/2010. hawa ni kutoka Kanda ya Kaskazini.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/03/2009 | Permalink | Maoni 0
July 02, 2009
Warefu wooote sasa kikapu.
Huyu nae kama Hashim Thabit. Baada ya hashim kuwini katika mpira wa kikapu katika ligi ya NBA Marekani sasa walio na kimo chake wameanza kijitokeza kucheza kikapu.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/02/2009 | Permalink | Maoni 0
Father Kidevu asajiliwa M Pesa
Usajili Maalum kwa mtu maalum.
Mkurugenzi Masoko wa Vodacom Epraim Mafuru akimshawishi Father Kidevu kujisajili na huduma ya M Pesa pamoja na kufanya usajili wa namba yake ya simu.
Mafuru amefanikiwa na sasa anaanza kujaza fomu maalum ya M Pesa. Kidevu akitia saini fomu hiyo ya usajili. Kidevu akielekezwa namna ya kutumia huduma ya M Pesa.
Kidevu akifuata maelekezo ya matumizi ya M Pesa.

Baada ya kukabidhiwa hati yake ya M Pesa, alisubiri kupata ujumbe wa kusajiliwa.
Akiweka Fedha katika acount yake ya M Pesa ambapo sasa ataweza kununua muda wa maongezi kwa njia ya M Pesa na kutuma fedha kwa ndugu na jamaa.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 7/02/2009 | Permalink | Maoni 0
June 30, 2009
Karibu Sasatel na ujionee mambo yetu.
Meneja Maoko wa Kampuni mpya ya simu za mkononi ya Sasatel, Derick Byarugaba (kulia) akimwelezea mmoja wa watembeleaji wa maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, Hassan Kihago namna simu zao zinavyo fanya kazi jana katika banda lao lililopo katika maonyesho hayo.
Wafanyakazi wakijadiliana jambo wakati wa maonyesho.
Mrembo wa Costomercare akisubiri wateja kwa tabasamu la ukarimu.
Mawakala wa Sasatel, BlueStar nao wapo katika banda hilo katika viwanja vya Sabasaba.
Wateja wakitembelea banda la Sasatel na kujipatia simu za mezani kwa bei nafuu, Muda wa maongezi na simu ya mkononi bure.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 6/30/2009 | Permalink | Maoni 0
June 29, 2009
Cheyo atimuliwa Bungeni na Spika
Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo akitoka nje ya ukumbi wa Bunjge Mjini Dodoma Juni 29, 2009 baada ya kuamriwa kufanya hivyo na Spika wa Bunge Samwel Sitta kwenye kikao cha jioni.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 6/29/2009 | Permalink | Maoni 2
wanafamilia waliokufa ajali ya mato waagwa.
Baadhi ya waombolezaji wakipita kutoa heshima za mwisho kwa miili ya marehemu watano wa familia moja waliokufa kwa ajali ya moto mwishoni mwa wiki jijini wakati wa kuaga miili hiyo, Kigogo Mburahati jana.
 
© FATHER KIDEVU Tarehe: 6/29/2009 | Permalink | Maoni 0
 

Idadi ya watu