Nafasi Ya Matangazo

November 27, 2015


Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.


Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.

Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.

Habari kamili inaandaliwa. Fanya subira.... Kwa sasa anza na picha....
 Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Posted by MROKI On Friday, November 27, 2015 1 comment

1 comment:

  1. SASA KAZI TU ni baada ya HAPA KAZI TU ya mh JPM safi sana, na hii ni baada ya siku 20 tangu serikali ya 5 ianze kazi inaonekana uchumi umeanza kupanda kwa speed ya ajabu balaa du, sasa nasema hivi JPM NA MHM waendelee na uzi huo huo sisi huku tunafunga na kuomba uklinzi na busala na hekima na ujasili na nguvu kwa Mwenyzi Mungu ziwe zaidi na zaidi juu yao AMEN, hakuna kurudi nyuma pigeni kazi kwa ujasili wotw

    ReplyDelete

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo