Nafasi Ya Matangazo

November 27, 2015

Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U15) imeingia kambini jana jioni katika hosteli za TFF zilizopo Karume jijini Dar es salaam, kujiandaa na ziara ya mafunzo katika ukanda wa Afrika Mashariki itakayoanza Disemba Mosi mwaka huu.

Kocha wa timu hiyo Sebastian Mkomwa amesema vijana wote wameshawasili jijini Dar es salaam na leo wameanza mazoezi asubuhi katika uwanja wa Karume watakapokua wanajifua kila asubuhi na jioni mpaka siku ya safari.

Kikosi cha wachezaji 24 kimeingia kambini kujifua na ziara ya Afrika Mashariki, ambapo timu hiyo inaandaliwa kwa ajili ya kushiriki kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17, zitakazofanyika mwaka 2017 nchini Madagascar.

Timu ya Taifa ya vijana imeakua na program ya kukutana kila mwisho wa mwezi kwa ajili ya kufanya mazoezi na kucheza michezo ya kirafiki na timu za kombani za U15 katika mikoa mbalimbali nchini, ambapo kwe mwezi Disemba itakua pamoja kwa wiki tatu katika nchi za Afrika Mashariki ikicheza michezo ya kirafiki.

Disemba Mosi, U-15 itasasiri kuelekea jijini Mwanza ambapo itacheza mchezo mmoja wa kirafiki na kombani ya jijini Mwanza (U17), kasha kusafiri kueleka mkoani Kigoma itakapocheza michezo miwili dhidi ya kombaini ya mkoa wa Kigoma (U17) na timu ya Taifa ya Burundi (U17).

Ziara hiyo itaendelea katika jiji la Kigali kwa kucheza michezo miwili dhidi ya timu ya Taifa ya Rwanda (U17), Jinja dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda (U17), Nairobi dhidi ya timu ya Taifa ya Kenya (U17) na kumalizia kwa mchezo dhidi ya kombaini ya mkoa wa Arusha (U17) na kurudi jijini Dar es salaam.
Posted by MROKI On Friday, November 27, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo