Nafasi Ya Matangazo

September 02, 2015

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (katikati) kwa kushirikiana na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto) na Mama Zakhia Meghji (kulia) wakiweka shada la maua kwenye kaburi LA Marehemu Hulda Kibacha aliyezikwa katika makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akishiriki kwenye ibada ya kumwombea Marehemu Hulda Kibacha, Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA iliyofanyika nyumbani kwa marehemu eneo la Ada Estate tarehe 2.9.2015. Aliyekaa kushoto kwa Mama Salma ni Mheshimiwa Zakhia Meghji na kulia ni binti wa marehemu Nampombe Kibacha
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mdhamini wa Taasisi ya WAMA Mama Hulda Kibacha aliyefariki dunia tarehe 28.8.2015 hapa Dar Es Salaam. Marehemu Kibacha aliwahi kufanya kazi Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka udongo kaburini ulimolazwa mwili wa Mama Hulda Kibacha aliyekuwa Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA. Marehemu Hulda Kikbacha alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Hulda Kibacha.
Posted by MROKI On Wednesday, September 02, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo