Nafasi Ya Matangazo

July 01, 2015

Naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia na Mbunge wa Bumbuli, January Makamba akisalimiana na naibu Sheikh wa Mkoa na Msaidizi wa Kaadhi mkoa wa Mtwara, Kassim Kuneng'echa mara baada ya kwasili mkoani Mtwara. Januari Makmba alikuwapo mkoani Mtwara  katika ziara yake ya kusaka wadhamini watakaomuwezesha kupata ridhaa ya CCM kugombea kiti cha urais.
 Mh January Makamba akihutubia wananchi na wanachama wa CCM mkoani Mtwara waliojitokeza katika Viwanja vya ofisi ya CCM Wilaya ya Mtwara Mjini. January yupo katika ziara yake ya kusaka wadhamini ndani ya chama ambao watamuwezesha kuteuliwa kuwania nafasi ya urais wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM.
 Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akisalimiana na wananchi na wananchama wa CCM mkoa wa Mtwara waliojitokeza katika viwanja vya ofisi za CCM Wilaya ya Mtwara Mjini kumuunga mkono katika harakati zake za kusaka wadhamini mkoani hapo.
Mbunge wa Bumbuli na naibu waziri wa mawasilano, sayansi na teknolojia, January Makamba akiwapungia mkono wananchi na wananchama wa CCM mkoa wa Mtwara waliojitokeza katika viwanja vya ofisi za CCM Wilaya ya Mtwara Mjini mara baada ya kuwasili kwenye viwanja hivyo, Makamba alikuwa Mkoani Mtwara katika harakati zake za kusaka wadhamini mkoani hapo.
Posted by MROKI On Wednesday, July 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo