Nafasi Ya Matangazo

May 19, 2015

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Jacinto Nyusi kwenye Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma.
 Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Jacinto Nyusi akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kuwasili kwenye Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.

 Baadhi ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ,pamoja na viongozi wengine wa CCM mkoa wa Dodoma wakiimba wakati wa kumkaribisha Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi kwenye makao makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa neno la kumkaribisha Rais wa Msumbiji na Mwenyekiti wa Chama cha Frelimo Mhe. Filipe Nyusi kwenye makao makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais wa Msumbiji kuhutubia viongozi mbali mbali wa CCM wakiwemo baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu
 Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu, Viongozi wa CCM mkoa wa Dodoma pamoja na wageni waalikwa wakisikiliza hotuba ya Rais Filipe Nyusi kwenye ukumbi wa NEC mjini Dodoma.
 Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi akihutubia kwenye ukumbi wa NEC ,Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi akijaribu kofia ya CCM ikiwa sehemu ya zawadi alizopewa na CCM.
 Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi pamoja na Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa mjini Dodoma
Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi akiwaaga wana CCM mara baada ya kuwahutubia ambapo alisisitiza kuwa Frelimo itaendelea kudumisha mshikamano wao na CCM.
Posted by MROKI On Tuesday, May 19, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo